Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda akipokea mfano wa hundi ya shilingi
milioni 15 kutoka kwa Robert Pascal Mkuu wa Kitengo cha Kilimo benki ya
NMB, kama mchango wa benki hiyo kwa ajili ya kununulia madawati ya
shule za msingi katika mkoa huo, Ikiwa ni mchango wa benki hiyo katika
maendeleo ya elimu Mkoani Katavi, ambao umezinduliwa rasmi na Makamu wa
Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal kwenye viwanja vya Kashaulili mjini
Mpanda, na kuhudhuriwa na wananchi wengi wa mkoa huo. Mbali
na fedha hizo benki ya NMB pia imetoa kiasi cha shilingi milioni 15
zingine na vifaa vya michezo ikiwemo mipira na jezi kwa ajili ya timu za
mpira wa miguu za mkoa wa Rukwa na Katavi kwa ajili ya kufanikisha
mchezo wa mpira wa miguu kati ya timu hizo wakati wa uzinduzi katika
mkoa huo , pamoja na maandalizi mengine ya shughuli za uzinduzi, jumla
ya fedha iliyotolewa na Benki ya NMB ni shilingi milioni 30 za
Kitanzania.
Makamu
wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal akizungumza na wafanyakazi wa benki
ya NMB wakati alipotembelea banda la benki hiyo katika maonyesho
yaliyofanyika wakati wa uzinduzi wa mkoa mpya wa Katavi mjini Mpanda.
Makamu
wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akiteta jambo na Waziri
Mkuu,Mh. Mizengo Pinda, wakati wa kutathmini mrejesho wa kongamano la
Uwekezaji katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika Oktoba 17 mwaka
jana mjini Mpanda.
Mkuu
wa mkoa wa Katavi Dkt Rajab Rutengwe akikaribisha wageni mbalimbali
waliofika kwa ajili ya uzinduzi wa Kongamano hilo na Mkoa wa Katavi
lililofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya Maji Mjini Mpanda hivi karibuni.
Monday, November 26, 2012
BENKI YA NMB YACHANGIA MILIONI 30 KUFANIKISHA UZINDUZI WA MKOA WA KATAVI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment