Wednesday, January 2, 2013

MR & MRS KAMNA WAPATIKANA USIKU WA MWAKA MPYA TABORA

 Katika ni mshindi wa kwanza wa shindano la Miss Kamna,Mariam Wilfred akifuatiwa na mshindi wa pili kulia ni Mwasiti Thabit,kushoto ni mshindi wa tatu  Sabrina Michael.
 Baadhi ya washabiki waliofurika katika ukumbi wa Theophilo Kisanji wakiwa wanashuhudia mashindano ya kuwasaka Mr. na Mrs Kamna usiku wa mwaka mpya.
 Washindi wa tano bora wakiwa Jukwaani mara baada ya kutangazwa wakisubiri kuulizwa maswali ili kujiongezea idadi ya point katika mashindano hayo yaliyokuwa na mvuto mkubwa.
 Majaji walikuwa na kazi ngumu ya kuhesabu na kutoa point kwa washindi katika mashindano hayo
 Huyu ndiye Mr.Kamna 2013 Daniel Kisanga muda mfupia mara baada ya kutangazwa mshindi katika mashindano hayo.
 Washindi wa tano bora kuwania Mr.Kamna 2013 wakiwa jukwaani wakisubiri maswali ya kizushi ambayo kwakweli yalikuwa ni mtihani mkubwa kwao.
 Washabiki
 Mkuu wa wilaya ya Tabora Suleiman Kmchaya akicheza muziki wakati wa mashindano hayo akiwa na Naibu Meya manispaa ya Tabora Waziri Mrenda kulia,na kushoto ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora Moshi Nkonkota,ilikuwa ni mara baada ya kutimu saa sita kamili usiku hii ilikuwa ni ishara ya kuupokea mwaka mpya wa 2013. 
Hawa ni baadhi ya wadau wa TABORALEOHABARI.COM wakiwa katika moja ya pozz la picha ya pamoja wakati wa mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment