Thursday, January 17, 2013

SHULE YA MSINGI YA KAB ILIWAA NA UHABA WA MATUNDU YA VYOO .

Na Lucas Raphael.Nzega.



ZAIDI  ya  Wanafunzi  1500  wa  shule  ya  msingi   Nyasa  mbili  iliyopo  wilayan i Nzega  Mkoani  Tabora wanakabiliwa na uhaba wa matundu ya vyoo.

Akizungumza  na   waandishi wa habari ofisini kwake jana mwalimu  mkuu  wa shule  hiyo  George  Alphonce  alisema kuwa  shule  hiyo  ina wanafunzi  1520 huku   ikiwa na  matundu  ishirini  ya  vyoo  ambayo  haya tosherezi  kwa  matumizi  ya  wanafunzi   hao.

Alisema  kuwa  kwa  idadi  hiyo  shule  inaupungufu  wa  matundu  40 ambapo  kwa  sasa  wanafunzi   hao  hutumia  tundu  mmoja  wanafunzi  76  nje  ya  utaratibu  wa  kawaidi ,utaratibu  wa kawaida inapaswa  tundu  mmoja  wanafunzi  20.

Alisema  kuwa  tatizo hilo  ni  la muda  mrefu   kutokana  na  kuongezeka  kwa  wanafunzi  kila  mwaka  tofauti  na  wale  wanao  hitimu  elimu  ya  msingi ya Darasa la saba.

George  alisema kuwa wanafunzi kwa kipoindi hiki wanap[ata shida kujisaidia katika matundu hayo  hali ambayo wanajikuta wakiwa katika wakati mgumu na kusababisha mazingira ya kusoma kuonekana kuwa magumu kutokana na uhaba huo wa matundu.

Alisem,a Jitihada inayofanika kwa kushilikiana na kamati ya shule pamoja na wazazi wapo katika harakati za kukamilisha matundu ya vyoo nane ambayo yatasaidia kupunguza msongamano huo.

Alisema wazazi na walezi wamejitokeza kupambana na tatizo hilo ili kuhakikisha wanafunzio hao wana soma katika mazingira mazuri.

George aliomba serikali kuingilia kati suala hilo kuhakikisha wananfunzi wana soma katika mazingira stahiki ili kuwawezesha kufanya mazuri katika mitihani yao ikiwa na kukarabati miundombinu mbalimbali ya masomo katika shule za msingi.

Aliongeza kuwa wazazi wajitokeze kwa wangi kusaidia serikali katika kuboresha mazingira ya kusoma watoto wao ikiwa na kuchangia michango m,b alimbali ya shule.

Mkuu wa wilaya ya Nzega ,Bituni Msangi alisema kuwa jitihada zinaendelea kuwa hamasisha wazazi na walezi katika kuchangia maendeleo na kutatua matatizo ya wanafunzi ambayo yapo katika uwezo weao ikiwa na kuboresha mazoingira ya masomo pamoja na vyoo.

Mkuu huyo wa wilaya  alisema kuwa taarifa hiyo itafuatiliwa kwa Ofisa Elimu wilaya ili suala hilo liweze kufuatiliwa kwa ukaribu ikiwa na kukagua mazingira mbalimbali ya shule hizo pamoja na vyoo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment