Saturday, January 12, 2013

WATUMISHI WA SERIKALI NA ASKARI POLISI WANALANGUA TUMBAKU-WAKULIMA



NA LUCAS RAPHAEL,TABORA
 
MWENYEKITI wa chama cha mapinduzi,(CCM),Hassan Wakasuvi,amesema kilimo cha tumbaku mkoani Tabora,wakulima wake wataendelea kuumia kufuatia baadhi ya watumishi wa serikali, na askari polisi kujiingiza katika ulanguzi wa zao hilo katika kipindi cha masoko.
 
Wakasuvi alisema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake hivi karibuni baada ya mkutano mkuu wa chama kikuu cha wakulima wa tumbaku kanda ya magharibi,(WETCU),mkoani humo.
 
Alisema hali ikiendelea itafikia mahali zao la kumnufaisha mkulima itakuwa ndoto hivyo ni vyema serikali ya mkoa ikafuatilia hilo na kulifanyika kazi ili haki za wakulima zionekane na siyo ilivyo sasa.
 
“Katika mkutano mkuu wa WETCU ambao uliambatana na uchaguzi,mkuu wa uongozi wake, wapo wakulima waliotoa kero ya baadhi ya watumishi wa serikali na askari polisi wanajihusisha na ulanguzi wa zao la tumbaku.” Alisema.
 
Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa kufuatia wakulima hao kulalamika hayo,hata yeye ameshafanyika kazi lalamiko hilo na kuona ipo haja ya kuweka wazi tatizo hilo ili kuondoa dhuluma iliyopo ikiwezekana kuwataja kwa majina endapo wataendelea na biashara hiyo.
 
Alisema amewasilisha kilio hicho kwa mkuu wa mkoa wa Tabora,Fatma Mwassa ili aweze chukua hatua stahiki dhidi ya watumishi wa serikali na serikali wanaojihusha na ulanguzi wa tumbaku ambapo mkuu huyo wa mkoa amesema atafuatilia kwa ukaribu na kuchukua hatua.
 
Wakasuvi aliongeza kuwa yupo tayari kumtetea mkulima yoyote kati ya wale waliotoa malalamiko yao mbele ya mwenyekiti wa WETCU Alcard Iragila kuwa kuna watumishi wa serikali na askari polisi wanalangua tumbaku kipindi cha mauzo na masoko.
 
“Tuhuma hizi ni za kweli wala hakuna haja ya kusingizia mtumishi wa serikali ama askari polisi……siyo majungu ni tuhuma za ukweli na tutapigania hili hadi mwisho na tabia hii ya dhuluma kukomeshwa kabisa.”alisema 
 
Alisema kuwa anajua kuwa wakulima waliothubutu kutamka kuwa askari polisi na baadhi ya vigogo wa serikali wanalangua tumbaku kipindi cha masoko ya zao hilo watasumbuliwa, lakini anaamini kuwa anawatetea kwa nguvu zote hadi pale haki inapatikana.

No comments:

Post a Comment