Wednesday, September 26, 2012

RADI YAUA WANAFUNZI DARASANI

Na Lucas Raphael,Tabora

MWANAFUNZI mmoja wa darasa la 3 katika shule ya msingi msiliembe amekufa hapohapo baada ya kupiga na RADI na wangine 23 wajeruhiwa na watano wamelezwa katika hospital ya mkoa kitete kwa matibabu zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana (leo)Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Edward Bukombe alisema kwamba tukio hilo septemba 25 mwaka huu ,katika kijiji cha msiliembe kata ya mabama , majira ya saa 8 alasiri katika shule ya msingi msiliembe wilaya ya Uyui mkoani hapa

Kaimu kamanda huyo alimtaja aliyefariki kuwa ni Husna Ramadhani (10) aliyekuwa akisoma darasa la tatu katika shule akiwa na wenzake daasani wakati mvua hiyo ilipoanza .

Bukombe alisema kwamba wakti mvua hiyo ilipoanza kunyesha ikiambatana na radi wanafunzi wa darasa la tatu na nne wote walikuwa wamekaa kwenye chumba kimoja cha darasa wakiwa wanaendelea kujisomea ndio radi hiyo ilipopinga na kusabisha kifo hicho.

Kaimu kamanda huyo wa jeshi la polisi mkoani Tabora alisendelea kusema kuwa watoto wengene 23 waliuokuwepo ndani ya darasa hilo nao walipata madhara ,lakini watoto 5 walipata madhara makubwa na kulazimika kulazwa katika hospital ya mkoa kitete kwa ajili ya matibabu .

Aliwataja waliozwa kuwa ni Bundala Juma (10) wa Darasa la nne ambaye ameumia kwenye macho hayaoni vizuri,Hamisi Mashaka(10) anayesoma darasa la tatu,Cresesia Simon (12) mwanafunzi wa darasa la nne,Kwangu Luone (12) anayesona darasa la nne na Zaituni Ally(10) mwanafunzi wa darasa tatu.

Alisema kwamba wanafunzi walijeruhiwa wanaendelea na matibabu katika hospia; hiyo na wanendelea vizuri kwa mujibu wa taarifa waliopata asubuhi hii kutoka kwa daktari wa mkoa .

Hata hivyo kaimu kamanda bukombe amewataka walimu  kuakikisha wanafunzi mara baada ya kuona mvua zinaaza kunyesha basi wanatakiwa kuingia madarasni kwa ajili ya kuepuka radi za aina hiyo.

mwisho

No comments:

Post a Comment