Friday, September 21, 2012

WIKI YA USALAMA BARABARANI MKOANI TABORA


Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa akikata Utepe ikiwa ni Ishara ya ufunguzi wa Wiki ya  Nenda kwa usalama barabarani mkoani Tabora,kutoka kushoto ni Kamanda wa kikosi cha Usalama barabarani  SSP Hamisi Kisandu,Mbunge wa jimbo la Tabora mjini Bw.Ismail Rage na kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora mjini. 

Baadhi ya askari wa usalama barabarani wakiwa katika maandamano wiki ya Usalama iliyofanyika Stendi mpya ya mjini Tabora.


Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani  mkoa wa Tabora SSP Hamisi Kisandu akisoma risala fupi katika hafla ya ufunguzi wa wiki ya usalama barabarani.

Maandamano ya Bajaji za mizigo yakipita mbele ya mgeni rasmi katika hafla hiyo.

 Mkurugenzi mkuu wa kampuni la usafirishaji la mabasi ya NBS Bw.Hamdani Nassor akiwatunza waimbaji wa kikundi cha kwaya cha Shule ya msingi ya Town School wakati walipokuwa wakitumbuiza katika hafla hiyo ya wiki ya usalama barabarani iliyofanyika kimkoa Stendi mpya ya mabasi mjini Tabora.

No comments:

Post a Comment