Tuesday, September 25, 2012

WANAFUNZI 4000 WASHINDWA KUFANYA MTIHANI WA HABARI


Na Lucas Raphael,Tabora

Wanafunzi wapatao 4000 katika wilayani Igunga mkoani Tabora wameshindwa kufanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba kutokana na sababu mbalimbali ikiwepo na vifo na  utoro unaochangiwa na wazazi wa watoto kuwatka kuchanga mifugo .

Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa wilaya ya Igunga Elibariki Kingu katika Mahafali ya pili ya Darasa la saba ya shule ya msingi ya sent Leo iliyopo wilayani Igunga.

Kingu alisema kuwa wanafunzi hao walianza wakiwa darasa la kwanza zaidi ya 12800 mpaka kuhitimu darasa la saba 8000 ambapo wanafunzi ambao hawakufanya mtihani wa kuhitimu darasa hilo walikuwa 4000.





Alisema kuwa wazazi wanatakiwa kuwafuatilia watoto wao pindi wanapo anza shule mpaka kuhitimu darasa husika ili kupambana na adui uchinga.

Alisema idadi hiyo ya wanafunzi 4000 kutofanya mtihani niidadi kubwa hivyo wazazi wanapaswa kubadili mara mmoja ili kuhakikisha kila mtoto anapata Elimu hiyo ya msingi.

Alisema kuwa mzazi atakaye bainika kuto mpeleka mtoto shule ama kuchangia mtoto kuto enda shule hatua kali zitachukuliwa ikiwa na kupelekwa mahakamani kwa mzazi husika atakaye bainika na tuhuma hizo.

’’wakazi wa Igunga badilikeni mjue uchungu wa Elimu kwa watoto wenu hivyo basi niabu kati ya watoto 12800 watoto 4000 hawajafanya mtihani hii haipendezi razima mzazi wajibishwe wazazi hawa ni wazembe,atakaye bainika hatua kari zitachukuliwa ikiwa na kufishwa mahakamani’’alisema Kingu.

Aliwaagiza viongozi wa vijiji,kata pamoja na viongozi wa dini kutoa hamasa kwa wananchi kuhakikisha watoto wanaandikishwa shule pamoja na kuwafuatilia watoto hao mpaka hatua ya mwisho ya mitihani yao.

Sababu mbalimbali zilizosababisha mpaka watoto hao kutofanya mtihani huo ni pamoja na utoro wa kupindukia,kuolewa kwa wan afunzi wa kike, shuguli za kiufugaji pamoja na shuguli za kilimo.

Meneja wa shule hiyo Coaster Olomi alisema kuwa wazazi wanapaswa kutambua umuhimu wa Elimu na kuwakazania watoto hao kupenda shule nakuongeza kuwa jamii za wafugaji zi Elimishwe zaidi ikiwa na kuachana na imani potofu ambazo bado mpaka sasa zinaendelea.

MWIsHO.



No comments:

Post a Comment