Tuesday, November 13, 2012

WATU SITA WAPANDA KIZIMBANI KWA WIZI WA MITIHANI


Na Lucas Raphael,Tabora


Watu sita walio vunja ofisi na kuiba mitihani ya kidato cha pili katika  shule ya sekondari Bukene wilayani Nzega Mkoani Tabora wamefikishwa mahakamani jana na kwa kujibu tuhuma hizo zinazo wakabili.

Watuhumiwa hao sita wakiwepo na wanafunzi watatu walifikishwa mbele ya mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Nzega Nov,12 mwaka huu kwa tuhuma za kuvunja ofisi ya mwalim mkuu na kuiba mitihani mitatu ya taifa ya kidato cha pili ambayo inayoendelea kufanywa na wanafunzi wa kidato hicho  sehemu mbalimbali hapa nchini.

Mwendesha mashitaka wa polisi Merito Ukongoji akisoma mashitaka hayo mbele ya hakim mkazi Joseph Ngomero kuwa watuhumiwa hao wanatuhumiwa kwa kuvunja ofisi ya mwalimu mkuu wa  shule ya sekondari Bukene iliyokuwa ikihifadhi mitihani hiyo Nov 9 mwaka huu majira ya saa 2 usiku hadi saa 6 usiku.

Ukongoji aliwataja watuhumiwa hao sita wakiwepo na wanafunzi watatu kuwa ni charles fabiani(48) ambaye alikuwa mlinzi wa ofisi ya mwalim mkuu,Thabiti saidi(20) mkazi wa Bukene,Rashidi shaibu(18) m kazi wa bukene.

Katika tuhuma hiyo wanafunzi wakiwa ni salehe matongoro(17) mwanafunzi kidato cha tatu shule ya sekondari kili, Matius Daudi (16)pamoja na Abdalallha Hamis(15) ni wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Bukene.

Kesi hiyo ikisikilizwa kwa Malaya ya kwanza imeahilishwa mpaka Nov 19 mwaka huu itakapo sikilizwa kwa mala ya pili.

Mitihani iliyoibiwa na watuhumiwa hao ni mitatu ikiwepo na mtihani wa Physcs,Biology na chemistry hata hivyo kwa mujibu wa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya nzega Kyuza kitundu alisema kuwa udhibiti mkali ulifanyika kuhakikisha mitihani hiyo haikufika kwa shule jirani zilizoko karibu na tukio hilo lilipo tokea.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment