Sunday, November 25, 2012

MAOMBOLEZO YA KIFO CHA POLEY AHMED


Fahim Ahmed au maarufu Poley ambaye alizaliwa mnamo mnamo mwaka 1959 katika hospitali ya Kalunde hapa manispaa ya Tabora.

Mwaka 1972 alimaliza shule ya msingi Isike na hatimaye kuanza elimu ya Sekondari 1973 katika Shule ya Sekondari ya Uyui hapa hapa Tabora.

Baadaye aliondoka na kwenda Uingereza ambako alipata elimu ya juu na hatimaye kurudi tena nchini kuendeleza gurudumu la maendeleo.

Ni mengi aliyoyafanya mbali na kutoa michango yake kwa Serikali ya Tanzania kama mzalendo na hasa alipoamua kutoa ajira kwa vijana na wazee pasipo kujali rangi wala kabila.

Poley au Fahim ni dhahiri alifanya yaliyoonekana hata kufikia hatua ya kuleta ishara njema ya mabadiliko katika mkoa huu ambao maendeleo yake yalikuwa yakitajwa kuwa yanakuja kwa kusuasua sana.

......  Pumzika kwa amani,...Tutazidi kukukumbuka katika jitihada zako za kuleta maendeleo mkoani Tabora.

No comments:

Post a Comment