Thursday, November 29, 2012

SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WATAALAM WA KUREKEBISHA UPEO WA MACHO KUONA,PIA YAKABIDHI MAGARI 9 NA PIKIPIKI 107 KUSAIDIA HUDUMA ZA AFYA NCHINI


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wataalam wa Kurekebisha Upeo wa Macho Kuona nchini leo jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la wataalam wa kurekebisha upeo wa macho kuona nchini Adam Simbeye (kulia) akiwaeleza wajumbe malengo ya baraza hilo ya kusimamia, kudhibiti na kuratibu utoaji wa huduma bora za macho nchini yanayofanywa na baraza hilo kwa mujibu wa sheria ya Optometria Na.12 ya mwaka 2007. Kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi.
Wajumbe wa Baraza la Wataalam wa Kurekebisha Upeo wa Macho Kuona nchini wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi (Katikati) mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza hilo leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dkt. Hussein Mwinyi (kushoto) na mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan (kulia) kwa pamoja wakisaini nyaraka za kukabidhi magari 9 ya kubebea wagonjwa na pikipiki 107 kwa ajili ya kupelekwa katika maeneo mbalimbali kusaidia huduma za afya.
Mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan (kulia) akimkabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi (kushoto) akimkabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Bukombe Dkt.Archard Rwezahura (katikati) leo jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan.Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.

No comments:

Post a Comment