Sunday, November 25, 2012

TUWASA WAWAKARIBISHA MVP KATIKA KUSHEHEREKEA SIKU YA FAMILIA

 Mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Tabora Tuwasa,Mzee Misigalo akikagua timu za wachezaji wa Tuwasa na Mvp wakati wa tamasha la siku ya familia.
 Mzee Misigalo akitoa pongezi kwa kiongozi wa mradi wa vijiji vya Milenia Mbola Mvp Dr. Gerson Nyadzi kwa kukubali kushiriki wafanyakazi wa Mvp katika siku hiyo ya familia ya Tuwasa.
 Michezo ya kukimbia kwa magunia
 Meneja masoko wa Tuwasa Bernard Biswalo akicheza mpira na mtoto wake katika kuadhimisha siku hiyo.
 Patashika ilikuwa hapa hadi kamba ilikatika zaidi ya mara mbili na hatimaye ushindi kupatikana kwa wafanyakazi wa Tuwasa.
 Timu ya wafanyakazi wa Tuwasa katika picha ya pamoja wakati wa michezo hiyo ya kujenga mahusiano baina ya Tuwasa na Mvp.
 Fadhila Lemba mchezaji wa timu ya valleyball ya Mvp akionesha uwezo wake katika mchezo huo.
 Kiongozi wa mradi wa vijiji vya Milenia Mbola Mvp Dr.Gerson Nyadzi akionesha uwezo wake katika kusakata kabumbu.
 Wafanyakazi wa Mvp.
 Mchezaji wa timu ya riadha ya Tuwasa,Sara Gela akimalizia mbio za mwisho za vijiti zilizompa ushindi dhidi ya timu ya Mvp.
 Fadhila Lemba akiwa amepata ushindi wa kwanza mashindano ya mbio fupi.
 Timu ya wanariadha wa Tuwasa.
 Shida Zebedayo akiwa amepata ushindi katika mbio za kufukuza kuku.
Hapa ilikuwa kazi kati ya wajumbe hawa wa bodi wakati wakikimbiza kuku,kushoto ni katibu wa CCM mkoa wa Tabora Idd Ame na diwani wa kata ya Ndevelwa Suleiman Maganga.

No comments:

Post a Comment