Thursday, November 29, 2012

WEKEZENI ELIMU KWA WATOTO WENU MWASSA


Na Lucas Raphael ,Tabora 

wekezini kwenye elimu ya watoto

Wazazi na walezi mkoani Tabora wametakiwa kuwekeza kwenye elimu ya watoto wao kwa kufanya hivyo watakuwa wamewapata urithi wa pekee watoto wao ,urithi huo ni mzuri kuliko mali .

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Tabora Fatuma Mwassa wakati wa mahafali ya kwanza ya shule ya msingi ya Istiqaama inayomilikiwa na taasisi ya kiislamu ya Istiqaama yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo jana .
 
Alisema kwamba kuwekeza kwenye elimu kutawasaidia watoto wetu kuwa na akili ya kutafuta elimu na mali hata baada ya wazazi wao kuwa hapo duniani,kwani tumeona watu wengi wanawashia watoto mali lakini mali hizo zinatumiwa na watu wengine na watoto wanazidi kuteseka .

Alisema kwamba familia nyingi zimekuwa zitafuta mali bila kuwekeze kwa elimu ya watoto wao na mwisho wa siku watoto wanakosa elimu na mali walizoziacha kwani wanadhulumiwa na wale waliwaacha kusimamia mali hizo .

Mwassa alisema kwamba iwapo wazazi watawaachia elimu watoto wao ni vizuri na hakuna mtu wa kudhurumu elimu hiyo zaidi ya mtoto huyo kuitumia kwa maufaa yake na taifa kwa ujumla .

Alisema kwamba hakuna mtu  ambaye hajui umuhimu wa elimu kwa maana hiyo kila mtoto anatakiwa kupata elimu iliyobora kwa ajili  ya kukabiliana na soko la ajira.

Hata hivyo mkuu huyo wa mkaow a Tabora alifanikisha kuongoza harambee na kuichangia kiasi cha shilingi milioni 25,fedha zilizopatikana zitasaidia kukamilisha ofisi na madarasa ya wanafunzi  

Katika mahafali hayo watoto 42 wa eli mu wa hawali walipatiwa vyeti kwa ajili ya kujiunga na darasa la kwanza mwakani.

Awali shekhe wa mkoa wa Tabora Shabani Salum aliwataka wakazi wa mkoa wa tabora kuwekeza mkoani hapa tofauti  na watu wengine ambao wanawekeza katika mkoa wanayotoka .

Alisema kwamba imekumekuwe[po kasumba ya baadhi ya watu hasa wa mkoa huu kushindwa kuwekeza katika mkoa wao na kuwekeza katika mikoa mingine ,aliomgeza kuwekeza huo sio tatizo bali na msisahua kwenu.

Mwisho

No comments:

Post a Comment