Thursday, November 1, 2012

BREAKING NEWSSSSS.....NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO TABORA MJINI

Nyumba wakati ikiwa imeshika moto majira ya saa saba mchana leo hii licha ya juhudi kadhaa kutoka kwa kikosi cha zima moto kwa kushirikiana na wananchi kuzima moto huo uliodumu kwa zaidi ya saa mbili.

 Baadhi ya askari wa jeshi la Polisi walifika kwa wakati wakisaidia hali ya ulinzi na usalama katika ajali  hiyo ya moto ambapo hakuna mtu aliyepoteza maisha.

 Baadhi ya watu wanaoishi katika nyumba hiyo wakiwa na majonzi huku wakishuhudia wasamalia wema kwa kushirikiana na kikosi cha zimamoto wakiendelea na kuzima moto huo.

 Wananchi wakiwasaidia askari wa kikosi cha zimamoto kukabiliana na moto huo uliokuwa umeshika kasi na kuteketeza idadi kubwa ya mali zilizokuwapo ndani ya nyumba hiyo.

 Kamanda wa kikosi cha zimamoto Tabora Surgent Maganga Mgombele akijaribu kutoa utaratibu wa kuzima moto huo.
 Moja kati ya sare za askari wa JWTZ ambazo zimeteketea katika ajali hiyo mbaya inayodaiwa kuwa imetokana na hitilafu ya umeme.

No comments:

Post a Comment