Tuesday, December 25, 2012

Fichuka Development Agency yatambulisha mfumo mpya wa usambazaji wa kazi za wasanii

Kampuni ya Fichuka Development Agency Ltd, leo tarehe 21/12/2012 inatambulisha mfumo mpya kabisa  wa usambazaji wa  kazi za wasanii ambao umepewa jina la MFUMO RAFIKI (Code number) na utaanza kutumika rasmi kuanzia tarehe 23/12/2012 siku ya uzinduzi wa BUM KUBAM DVD utakaofanyika katika ukumbi wa New maisha Club ikiwa ni sehemu pia ya kuutambulisha mfumo huu mpya, tunaanza na msanii wa muziki  wa
kizazi kipya aina ya Hip hop Tanzania Nikki wa Pili katika Makala (Documentary) ya wimbo wake iliyopewa jina la BUM KUBAM DVD.

Bum Kubam inafungua njia ya mpya na ya kimaslahi kwa wasanii wa Muziki pamoja na Filamu nchini Tanzania, ikiwa ndio sekta pekee ambayo inakisiwa kuwa na uwezo mkubwa wa kutoa ajira kwa Vijana na rika lolote lakini ajira hizi hazikuonyesha kuzaa matunda lakini ujio wa MFUMO RAFIKI (Code Number) uliofanyiwa utafiti kwa  kina kwa lengo la kuokoa kizazi hicho katika kupambana na Maharamia.

Teknolojia hii mpya imegharimu kampuni fedha nyingi ikiwa katika utafiti pia kuutengeneza mfumo wa mauzo kwa kutumia mfumo wa Digitali ambao ni wa kwanza kabisa kufanyika Afrika pengine hata Ulimwenguni, hadi leo unatambulishwa kwenu wanahabari na umma kwa ujumla, kama tulivyosema awali kuwa makala ya Bum Kubam ni kazi ya kwanza lakini baada ya mwezi pia tutangaza kazi inayofuata kwa mfumo kama huu wa mauzo.

Kwa utafiti uliofanywa  kwa zaidi ya miaka mitatu na muasisi/mkurugenzi  wa kampuni ya Fichuka Develoment Agency  Frank John akishirikiana na wataalam kutoka sehemu mbalimbali waligundua kwamba sababu za wasanii kutonufaika na kazi zao ni, kuwepo kwa bidhaa Bandia (Fake) sokoni, kukosekana njia rahisi ya msanii kujua mauzo halisi  ya kazi zake, kutopatikana kwa kazi ya msanii

No comments:

Post a Comment