Wednesday, December 12, 2012

VETA KANDA YA MAGHARIBI WATAKIWA KUTOA MAFUNZO NYENYE UBORA

 
MKUU WA WILAYA YA KALIUA MKANI TABORA BW,SAVERI MAKETA AKIWASILI KATIKA VIWANJA VYA VETA AKIPOKEWA NA MURUNGEZI NA MKUU WA CHUA CHA VETA TABORA

WA KWANZA KUSHOTO NI KAIMU MKUU WA CHUA CHA ULYANKULU NA ANYEFUTA NI MKUU WA CHUA CHA VETA MKOA WA TABORA BW,MAKONGORO

MKUU WA WILAYA YA KALIUA BW,SAVERI MAKETA AKISAINI KITABU CHA WAGENI

MKURUNGEZI WA VETA KANDA YA MAGHARIBI BIBI HILDEGARDIS BITEGERA AKIWA NA MGENI RASMI SAVERI MAKETA OFISINI KWAKE

MKUU WA WILAYA YA KALIUA ALIYEMWAKILISHA MKUU WA MKOA WA TABORA AKIELEKEA KATIKA UKUMBI WA MKUTANO TAYARI KWA AJILI YA KUFUNGUA MKUTANO

WADAU WA VETA AKISIKILIZA HOTUBA YA MGENI RASMI KATIKA MKUTANO WA WADAU NA WAAJIRI ULIOWASHIRIKISHA VIONGOZI MBALIMBALI KUTOKA MIKOA YA SHINYANA,KIGOMA,SIMIYU NA TABORA


MKUU WA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI MKOA WA TABORA AKIWA NI MMOJAWAPO KATIKA MKUTANO HUO WA WADAU

MKUU WA WILAYA YA KALIUA ,MKURUNGEZI WA VETA WAKIWA TAYARI KUANZA KWA MKUTANO HUO





HAPA MKURUNGEZI WA VETA AKISOMA RISALA MBELE YA MGENI RASMI


MKUU WA WILA YA KALIUA AKISOMA HOTUBA KWA WADAU MBALIMBALI WALIOTOKA KATIKA MIKOA MINNE YA KANDA YA MAGHARIBI




PICHA ZOTE NA MADILI  KWA MAWASILIANO ZAIDI KWA SIMU NAMBA 0754-845258

Na Lucas Raphael,Tabora


SERIKALI imeitaka Mamlaka ya Elimu ya mafuzo na ufundi Stadi nchini kanda ya magharibi VETA kuhakikisha kuwa mafunzo wanayoyatoa yanazingatia ubora kwa kutumia mitaala iliyoandaliwa na watalaam toka viwandani.

 

Agizo hilo limetolewa mjini Tabora, na mkuu wa mkoa wa Tabora Bibi Fatuma Mwassa wakati akifungua mkutano kati ya VETA na waajili kutoka mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Simiyu na mwenyeji mkoa wa Tabora katika hotuba yake iliyosomwa na mkuu wa wilaya ya kaliua Saveri Maketa.

 

Katika hotuba yake mkuu huyo wa mkoa amesema kwamba VETA ni lazima ihakikishe kuwa inaajiri walimu wenye sifa na ambao wanahudhuria mafunzo ya vitendo viwandani mara kwa mara sambamba na kuwepo na karakana bora zenye vifaa vinavyokidhi mahitaji ya watalaam.

 

Aidha Bi Mwassa amesema kuwa VETA wanawajibu kuhakikisha kwamba wahusika waliopo katika sekta rasmi na isiyo rasmi, wanapata ujuzi kwa gharama nafuu wanayoweza kumudu, na kuwa ujuzi huo uwe na tija itakayokidhi mahitaji ya soko la ajira ndani na nje ya nchi.

 

Mkuu huyo wa mkoa wa Tabora pia ameelezea umuhimu wa kusimamia ujenzi wa taifa kwa kuanzisha mafunzo ya maadili vyuoni ili vijana waweze kujitambua, kulinda afya zao, na ausalama wa maisha yao, lengo ni kuwezesha kuwa na nguvu kazi yenye afya nzuri uzalendo na maadili mazuri kwa taifa lao.

 

Kuhusu mafunzo kazini mkuu wa mkoa amewataka waajiri hao kutoa ushirikiano kwa VETA kwa kuwaruhusu watumishi wao na kuwapa mafunzo ya vitendo na pia kuchangia misaada mbalimbali ikiwemo mitambo kwa ajili ya kuimarisha mafunzo vyuoni kwa vitendo.

 

Awali mkurugenzi wa VETA kanda ya Magharibi Bibi Hildegardis Bitegera amemweleza mkuu wa mkoa kuwa VETa kanda yake, inamiliki vyuo vinne vya ufundi Stadi.

 

Amevitaja vyuo hivyo kuwa ni Chuo cha VETA Shinyanga chenye uwezo wa kudahili wanafunzi 400,  chuo cha VETA Tabora chenye uwezo wa kudahili wanafuzi 400,  chuo cha VETA Kigoma chenye uwezo wa kudahili wanafuzi 480 na chuo cha VETA Ulyankulu ambacho kinauwezo wa kudahili wanafunzi wapatao 280.

 

Mwisho.

 

1 comment: