Tuesday, December 4, 2012

JIDA WATOAN ELIMU YA MKUKUTA AWAMU YA PILI




NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

SHIRIKA la lilisilokuwa la kiserikali la  JIDA Tanzania mkoani Tabora limeanza kutoa mbinu kwa wananchi kuhusu ufuatiliaji wa mkakati wa Serikali wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini MKUKUTA awali ya pili.

Akizungumza na ukurasa huu Afisa uhusiano wa JIDA ,John Pinini amesema kwamba shirika lake kwa ufadhiri wa Foundation For Civil Society wameamua kutoa elimu hiyo ili jamii iweze kutambua umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kujiletea maendeleo miongoni mwao.

Pinini alisema kuwa lengo kuu la kutoa hiyo ni kuongeza uelewa na ujuzi kwa jamii kuhusu MKUKUTA pia hiyo na kutoa sauti zaidi ili mwananchi waweze kushiriki kwa juhudi na maarifa katika kazi za mandeleo kwenye maeneo wanayoishi.

Aidha alisema kwamba dhumuni lingine la kutoa mafunzo hayo ni kutaka wananchi waelewe mbinu za kufuatilia utekelezaji wa MKUKUTA na kwamba ni kutaka kuona fursa ya majadiliano ya kisera ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini kwa mwananchi wa kawaida inakuwepo.

Hata hivyo Pinini amebainisha yakwamba ushiriki mdogo wa wananchi pamoja na wadau, katika kupanga mipango ya maendeleo umepelekea Serikali kushindwa kufikia malengo yake ya mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasiini kwa wananchi wake.

Ameeleza kuwa iwapo wananchi hao watafahamu umuhimu wa kufanyakazi kwa badii na maarifa ikiwa ni pamoja na kuzalisha chakula cha kutosha uchumi kwa jamii unaweza kukua na kuwa na maisha bora kuliko ilivyo sasa.

Alisema kuwa ili kufanikisha malengo ya Milienia ya MKUKUTA awamu ya pili ni lazima kila mwanajamii awe mkulima, mfanyakazi, biashara, wavuvi, viongozi wa Serikali, mashirika ya hiyari, na wadau wa maendeleo washiriki kwa vitendo kusimamia utekelezaji na kutathimini maendeleo ya MKUKUTA.

Mwisho.




No comments:

Post a Comment