Thursday, December 27, 2012

TBL YAFANIKISHA UPANDAJI MITI 2600 MWANZA


 Mgeni rasmi katika kampeni ya Mradi wa Upandaji Miti jijini Mwanza, Henry  Mongi, akipanda mti  wakati wa kampeni hiyo katika moja ya mitaa ya jiji hilo.Anayeshudia kulia ni Afisa Ubora wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Caroline Muhonoli na wa pili kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mkuyuni, Fasheni Lugo. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia Tanzania.
 Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Steven Kilindo,  akifukia udongo kwenye shimo alilopanda mti wakati wa kampeni ya  upandaji miti jijini Mwanza mwishoni mwa wiki..Wanaoshuhudia katikati ni Meneja Ubora wa kampuni hiyo, Caroline Muhonoli na nyuma ya Kilindo ni  Diwani wa Kata ya Mkuyunim, Lugo Fashen.TBL imetumia zaidi ya milioni 30 kupanda miti 7000 katika mikoa ya Mwanza,Kilimanjaro na Mbeya. Kwa Mkoa wa Mwanza pekee imetumia sh. mil. 10 kupanda miti 2600.
 Meneja wa TBL Mwanza, Richmondx Raymond akipanda mti katika uzinduzi wa mradi  wa upandaji miti jijini Mwanza mwishoni mwa wiki, uliofanywa na kampuni  hiyo kwa kupanda miti 2600 kando kando ya barabara za Balewa, Kenyatta,  machemba na shule za sekondari Nyamaganana na Nyegezi na Kiwanda cha Bia cha kampuni hiyo.

No comments:

Post a Comment