Sunday, December 23, 2012

UBAKAJI WA WATOTO WAKIKE MKOANI TABORA NI TATIZO

 
Na Lucas Raphael,Tabora


WASTANI wa watoto wa kike ni saba wenye umri kati ya miaka tisa hadi kumi na tano hubakwa kila mwezi katika Manispaa ya Tabora.
       
Msaidizi wa Dawati la jinsia la Jeshi la Polisi Wilaya ya Tabora ,Ruth Emmanuel amesema watoto wanaobakwa wengi ni wakatiwakitoka kwenye harusi za mitaani na kumbi za sherehe . .

Aliyesema hayo wakati akitoa mada katika semina ya ya wajumbe kutoka kata 10 za manispaa ya tabora  juu ya haki ya mtoto iliyofanyika katika ukumbi wa mikutao wa kituo cha wanafunzi na kuandaliwa na asasi isiyokuwa ya kiserikali ya goodness orgazation
       
Ameeleza kuwa wastani huo ni ule tu unaotolewa taarifa polisi huku asilimia kubwa ya wanaotoa taarifa polisi, wakifungua kesi ili wapate matibabu na mara baada ya kupata matibabu huwa hawarudi kuendelea na kesi, wakiwa wametoa anuani za uongo.
       
Ruth Emmanuel amebainisha kwamba watu wenye kumbi za starehe ni miongoni mwa wanaochangia ubakwaji wa watoto kwa kuruhusu waingie kwenye kumbi kinyume cha sheria inayokataza watoto chini ya umri wa miaka kumi na nane kuingia kwenye kumbi za sharehe na kwamba elimu inabidi izidi kutolewa kwao ili wafuate sheria.
       
Kwa upande wake bibi maendeleo ya jamii, Manispaa ya Tabora Zena Kapama ametupa lawama kwa wazazi kuwa hawatoi umuhimu wa malezi kwa watoto wao na ndio maana huwaachia watembee ovyo hadi usiku wa manane na kupata matatizo.

Alisema kwamba malezi ni kusimamia madili ya watoto kwani bila kufanya hivyo hakika watoto watakuwa na malezi mbaya sana ,hakuna jinsi ya kuthibiti vitendo na mienendo mbalilmbali ya watoto mara wafikapo nyumbani .
       
Amewataka wazazi na walezi kutoa umuhimu kwa watoto wao ili wapate malezi bora na hivyo kuepukana na matatizo yakiwemo ya kubakwa.

Hata hivyo bibi maendeleo huyo alisema kwamba sio kila kitu unamtaka kuamuachia mtoto bali kunavitu vingine sio vya kumuachia mtoto pekee yake .



Mwisho

 .

No comments:

Post a Comment