Thursday, December 27, 2012

SIKU YA WACHAGA YAFANA SANA MJINI MOSHI



chagga day ilivyopambwa ndani ya zumbaland mjini moshi.


boda 2 boda wakiwajibika jukwani shoo ya chagga day moshi ndani ya zumbaland.


ommy dimpoz akiimba na washabiki chagga day moshi.


ommy dimpoz akimuimbisha mtoto shoo ya chagga day ndani ya zumbaland.


thecla mgaya 'aisha' wa mambo hayo alikuwemo ndani ay nyumba akifurahia chagga day pale zumbaland moshi.
baadhi ya wanamuziki wa serengeti band ya arusha kabla ya kutumbuiza tamasha la chagga day moshi ukumbi wa kisasa wa zumbaland.
mtoto akichorwa katika mashamsham ya chagga day ukumbini Zumba Land.
mkurugenzi uhuru museum akitoa historia ya kabila la wachagga.

Tamasha kubwa la kihistoria lililopewa jina la Chagga Day Cultural Festival 2012 - Moshi lilifanyika kwenye ukumbi wa ZUMBA LAND katika manispaa ya Moshi siku ya Jumamosi tarehe 22/12/2012 kuanzia saa sita mchana mpaka saa sita usiku na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa mji huo huku baadhi wakioongozana na familia zao.

Tamasha hilo lililotawaliwa na shangwe za mara kwa mara kutoka kwa wakazi wa mji wa Moshi waliofurika kwenye viwanja hivyo maarufu kwa michezo ya watoto, liliandaliwa na kampuni ya Myway Entertainment ya jijini Dar chini ya Mkurugenzi wake Paul Mganga na kudhaminiwa na kampuni ya bia (TBL) kupitia bia ya Safari Lager na kampuni ya vinywaji baridi (SBC) kupitia kinywaji chake murua cha Pepsi.

No comments:

Post a Comment