Monday, December 3, 2012

RAIS KIKWETE AAHIDI MSAADA WA BAJAJI KWA MLEMAVU MWENDO SAID WA LINDI VIJIJINI


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na mlemavu Bwana Mwendo Saidi katika kijiji cha Mandawa wilaya ya Lindi vijijini leo wakati Rais aliposimama kwa muda kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho ili kujua changamoto za kimaendeleo zinazowakabili.Mlemavu huyo alimweleza Mheshimiwa Rais Kuwa yeye na wenzake wawili wanaomba wapatiwe Bajaji ili kuanzisha mradi utakaowawezesha kujikimu kimaisha.Mheshimiwa Rais Kikwete aliridhia ombi hilo na kuahidi kutoa msaada huo mara moja.Rais Kikwete yupo mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo. Picha na Freddy Maro

No comments:

Post a Comment