Monday, December 3, 2012

MAMA SALMA AKABIDHI MSADAA WA BOTI NA ZANA ZA UVUVI KWA VIJANA WA LINDI

 

Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa msaada vifaa vya kwa wawakilishi wa kinduchi cha Mwambao Fishing Group katika bandari ya Lindi jana jioni.
Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa msaada vifaa vya kwa wawakilishi wa kinduchi cha Mwambao Fishing Group katika bandari ya Lindi jana jioni.
Mke Wa Rais Mama Salma Kikwete na viongozi wengine pamoja na wawakilishi wa kikundi cha Mwambao Fishing group waki vuta kamba kuzindua rasmi Boti ya kikundi hicho jana wakati wa sherehe za makabidhiano yaliyofanyika katika bandari ya Lindi jana jioni.
 ………………………………………………………
Na Freddy Maro,Lindi

 Vijana kikundi cha Mwambao Fishing Group  wa Mji ya Lindi wamemshukuru mke Rais mama Salma Kikwete baada ya kuwakabidhi Boti ya Uvuvi na vifa vyake katika hafla fupi iliyofanyika katika bandari ya Lindi jana jioni.

Akisoma risala kwa niaba ya wanachama wa kikundi hicho, Katibu Msadizi wa kikundi Bwana Jackson John Mnenje alitoa ahadi ya kutunza boti hiyo na na kuvitumia kwa malengo  waliyojiwekea ikiwamo kununua boti nyingine baada ya mwaka mmoja kutokana na faida itakayo tokana na biashara za uvuvi.

“Juhudi alizofanya Mama Salma, zinaonyesha jinsi anavyoguswa na hali ngumu ya maisha ya Watanzania na dhamira aliyonayo ya kutukwamua kutoka katika hali hii.Tunamshukuru Mungu kwani leo sisi tumebahatika na kujiunga na Watanzania wengi wanaofaidika na juhudi zake za kuboresha maisha ya Watanzania,” wanakikundi hao walisema katika risala hiyo.
Kutokana na bei kubwa ya vifaa hivyo, vijana hao wamesema kati ka risala yao kuwa, wasingeweza kamwe kununua vifaa hivyo bila msaada huo uliotolewa na Mama Salma Kikwete na kwamba utakuwa kichocheo kikubwa  cha kukabiliana na na changamoto  za maisha zinazowakabili.

Akizungumza kabla ya kukabidhi Msaada huo,mke wa Rais Mama Salma Kikwete alisema msaada huo ni utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2010 na 2015 inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuongeza kuwa ilani hiyo imetambua kuwa uvuvi ni moja ya sekta za uchumi ambazo hazijapatiwa msukumo wa kutosha.

“Kuongeza ufanisi na tija na kubadili maisha ya wavuvi ni moja ya Mapinduzi yanayolengwa katika ilani ya CCM ya 2010 -2015 na mpango uliopo ni wa kuimarisha ushirika wa makundi ya ujasiriamali ikiwa ni njia moja kubwa ya kuwawezesha  wananchi  wa kawaida kumiliki na kuendesha uchumi,” alisema Mama Salma.

Mama Salma amesema kuwa Taasisi anayoingoza ya Wanawake na Maendeleo WAMA itaendelea kuwasaidi wananchi katika maeneo yao ya kujenga ushirika ulio imara na unaojitegemea kiuchumi na unaoendeshwa na wao wenyewe katika misingi wa uwazi na uwajibikaji.

Mama Kikwete amesema pia kuwa WAMA  inalo jukumu la kuhamasisha na kutoa msaada wa hali na mali kwa wananchi na kuwawezesha kufikia malengo wali yojiwekea kwa kuwapatia nyenzo na vifaa mbalimbali,lakini wajibu wa kujiendeleza na kujisimamia unabakia  wa watu wenyewe.

Mke wa Rais amewahimiza wanachama wa Mwambao Fishing group kujenga mshikamano ili kikundi hicho kipate utulivu utakao wapa fursa ya kupanga mipango ya kujenga na kuimarisha kikundi na kufanya kazi kwa uwazi,kuaminiana na kupeana moyo.

Kikundi cha Mwambao Fishing Group chanye wanachama  25 kilianzishwa mwaka huu katika manispaa ya Lindi kutokana na ushari wa Mama Salma Kikwete aliyewashaur i vijana hao kuunda kikundi na kubuni mradi wa maendeleo utakao wasaidia  kuboresha masiha yao.

No comments:

Post a Comment