Tuesday, December 4, 2012

UKAME WAPIGA HODI TABORA



Na Lucas Raphael,Tabora  


KIWANGO cha mvua katika Mkoa wa TABORA kimeshuka kutoka wastani wa Milimita 1500 kwa Mwaka hadi kufikia Milimita 600 Mwaka huu, hali inayosababisha maeneo mengi ya Mkoa huo kupata ukame na kutishia kushuka kwa uzalishaji wa Mazao ya Chakula.

Kiwango hicho cha mvua kimeshuka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, lakini kwa Mkoa wa TABORA kiwango cha mvua kinaendelea kupungua Mwaka hadi Mwaka kutokana na uharibifu mkubwa wa Mistu unaofanywa na uvamizi wa shughuli za kibinadamu.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwassa amewahamasisha Wananchi wa maeneo yote yenye ukame kuanza kupanda mazao yanayostahimili ukame kama Mhogo, Mtama, Viazi vitamu na Alizeti na Ofisi yake itatoa mbegu bure za Alizeti na Mhogo kwa maeneo yenye mahitaji makubwa.

 Alisema kwamba licha wa kutoa mbegu hizo kwa wilaya ambazo zinahitajinmakubwa laikini aliwataka wananchi kukitumia chakula kilichonacho kwa sasa  kwa ugalifu mkubwa .

Alisema kwamba tayari hali siyo nzuri kulinangana na mvua ilivyo kwa sasa kwani bila kuchukuliwa kwa hatua za tahadhari hali itakuwa ni mbaya zaidi kwa jamii .

Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa amewataka wakuu wa wilaya kuwahimiza wananchi kulima mazao ambayo yastahili  ukame ilikukabiliana na tatizo ambalo linaweza kujitokeza baaday iwapo mvua itaendelea kuwa kama ilivyo sasa.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa TABORA ametoa Mizinga ya kisasa 130 ya kufugua nyuki yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni Tatu na laki tisa (Mil. 3.9) ili kuwawezesha Vijana kuendesha shughuli za ufugaji nyuki na kujikwamua kiuchumi na Kikundi cha Wafugaji nyuki cha IPOLE kimepewa mizinga 30 ili kukiwezesha kufuga kisasa. 

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya Ya Sikonge Hanifa Selengu na Katibu wa Kikundi cha Wafuga Nyuki Ipole Jabiri Nassoro wamesema Mizinga hiyo itawawawezesha kufuga kisasa na kupata Asali nyingi itakayowandoa katika umasikini.

Mwisho

No comments:

Post a Comment