Saturday, December 1, 2012

VIJANA 40 WAPATA MAFUNZO YA UJASILIAMALI




Na Lucas Raphael,Tabora


ZAIDI ya vijana 40 wa kata ya shigamba wilayani Nzega mkoani Tabora wamepatiwa mafunzo ya ujasiria mali na shirika la kazi Duniani (I L O) yatakayo wawezesha kuwapa mwongozo wa kufanya kazi zao za ujasiria mali kwa ufanisi zaidi. 

Baadhi ya Vijana hao waliopata mafunzo hayo  walisema kuwa mafunzo hayo yamewawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi tofauti na hapo awali walikuwa wakifanya kazi zao kwa kutumia mazoea.

Wakitoa pongezi kwa shirika hilo la kazi Duniani (I L O) kwa kuwewezesha mafunzo hayo ya wiki mmoja mpaka kuhitimika jana waliongeza kuwa wanauwezo mkubwa wa kufanya biashara zao bila kupata hasara kama ilivyo kuwa hapo awali. 

Wakitoa wito kwa serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali Vijana hao wameiomba kuiga mfano huo na kuendeleza mafunzo kama hayo kwa vijana ili kuwawezesha kuwa wajasiria mali wazuri ambao watafanya kazi bila kupata changamoto ikiwa na kupunguza wimbi la vitendo viovu. 

Walisema endapo mashirika mengine yataiga mfano wa shirika hilo yatasaidia kupunguza wimbi la ukosefu wa ajira na vijana wengi watajiingiza katika ujasiria mali iliwaweze kujiajiri wenyewe. 

Kwa upande wake mratibu wa mafunzo hayo, Wenceslaus Antony Msita aliwapongeza vijana hao kwa kujitolea kupata mafunzo hayo ambayo yatawasaidia katika kuendesha miradi yao ya ujasiria mali.

Akitoa maelezo jinsi vijana hao walivyo patikana alisema kuwa ni vijana wenye umri wa miaka 16 hadi 45 ambao wamepata mafunzo hayo.

Aliongeza kuwa mafunzo hayo yataendelea kutolewa na shirika hilo kwa kata mbalimbali ili kila kijana wa wilaya hiyo aweze kuwa mjasilia mali ikiwa na kuondokana na umasikini.

Antony aliwataka vijana hao kuzingatia mafunzo yote waliyopewa katika kipindi hicho cha wiki mmoja ili waweze kuwa wajasiria mali wa kujitegemea.

Alishirika hilo halinauwezo wa kuwakopeshe badala yake litazungumza na taasisi za kibenki ili vijana  hao waweze kukopeshwa na kuendesha miradi yao bila kupata hasara yeyote itakayo weza kujitokeza.

Alisema kuwa vijana hao wanauwezo kubwa wa kuendesha biashara na kuongeza kuwa taasisi hizo ziwakopeshe kwa liba nzuri iliwaweze kurejesha mapema mikopo hiyo na kuendelea na ujasiria mali wao.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment