Na Lucas Raphael,Sikonge
Tohara ya Wanaume.Baada ya upasuaj |
JUMLA ya wanaume 5,838 mkoani Tabora wamefanyiwa Tohara
katika kampeni maalum inayondeshwa na
asasi ya kiraia ,kupitia wizara ya afya na ustwi wa jamii,ikiwa na lengo la
kupunguza kasi ya maambukizi ya ukimwi kwa wanaume.
MBOO AMBAYO AJIFANYIWA TOHARA |
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Tabora
,Fatuma Mwassa wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika
kimkoa katika uwanja wa Tasaf wilayani Sikonge mkoani hapa.
Alisema kwamba kampeni hiyo ya Tohara kwa wanaume
inaweza kupunguza kasi ya maambukizi kwa kundi mmoja la wanaume, kwani kwa
kufanya hivyo tayari watakuwa wameokoa maisha ya kundi lingine la wanawake.
Alisema kuwa licha ya kufanyika kwa tohara bado
kampeni hiyo inaendelea katika wilaya zote za mkoa wa Tabora kwa lengo la
kuhakikisha huduma hiyo inawafikia wanaume wote wenye tatizo hilo.
Mwassa alisema katika kipindi cha januari mwaka
huu hadi septemba jumla ya watu 41,032 walipima afya zao kati ya hao wananume
walikuwa ni 19,531 na wanawake walikuwa 21 591 waliokutwa na maambukizi ni
3,136 ni wanaume na wananwake ni 1,812 sawa na asilimia 7.6
Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa tabora
akizungumzia changamoto mbalilmbali zinaukabili mkoa huu alisema kwamba ugonjwa
wa ukimwi ni kuongezeka kwa idadi ya watoto yatima na waishio katika mazingira
magumu.
Awali afisa uhamasishaji na usambazaji wa PSI mkoani tabora ,Gabriel
Setumbi alimwambia mkuu huyo wa mkoa kuwa kwa kipindi cha januari hadi novemba
mwaka huu wameweza kusambaza mipira ya kikie na kiume kiasi cha pakiti 1,618,704
ambayo ni sawa na katoni 3747 ambapo mipira ya kike ni pakiti 57,600 sawa na
katoni 320.
Aidha alisema kwamba Psi wamekuwa wakielimisha
jamii juu ya matumizi sahihi ya kondom kwa kupitia kwa njia ya sinema ambao hutoa
ujumbe juu namna ya kujikinga na kujiepusha na mambukizi ya ukimwi .
Setumbi aliendelea kusema kwamba asasi hiyo
imeweza kutembelea wilaya zote za mkoa wa tabora na takribani maeneo 65 ya
vijijini na kata mbalimbali wameyafikia na kutoa elimu ya ukimwi.
Mwisho
No comments:
Post a Comment