Tuesday, October 23, 2012

IBF YAWAHAMASISHA WATANZANIA KWENDA KUMSHANGILIA FRANCIS CHEKA NCHINI UJERUMANI

 

 Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba ya Uarabu na Uajemi linawahamasisha Watanzania wajitokeze kwa wingi kwenda kumshangilia Francis Cheka katika mpambano wake na Benjamin Simon wa Ujerumani.
 Mpambamo huo ambao utafanyika tarehe 18 November 2012 katika ukumbi wa Universal jijini Berlin nchini Ujerumani utawakutanisha miamba miwili iliyosheheni kila aina ya ujuzi wa kupigana.
 Watanzania wawe na tabia ya kuwaenzi wenzao wanapowakilisha taifa hili kama wenzetu wanchi nyingine kama Kenya na Uganda wanavyofanya. Mbali na watanzania watakaokwenda wakifuatana na Francis Cheka tokea nyumbani, pia watanzania wanaoishi nchini Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya kama Uingereza, nchi za Skandinavia, Ufaransa, Uholanzi, Hungary na nyingine wanaombwa kujitokeza kwa wingi ili waweze kumshangilia Mtanzania mwezao aweze kupeperusha bendera ya nchi yetu vizuri.
 
 Tayari mtangazaji maarufu wa ITV na Radio One “Maulid Baraka wa Kitenge” pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Jambo Concept inayomiliki magazeti ya Jambo Leo, City Sports Lounge, Jambo Magazine Brand Tanzania bwana Juma Abbas Pinto aliye pia mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wameshaonyesha nia ya kwenda Ujerumani kulitangaza pambano hilo kwenye vyombo vyao vya habari pamoja na kumshangilia Francis Cheka.
 Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) inahamasishwa pia itumie nafasi hii kuitangaza nchi yetu huko Ulaya kama zinavyofanya bodi nyingine kama za Kenya, Botswana, Uganda, Oman na nyinginezo zinazotumia wanamichezo wake kutangaza vivutio vya kitalii nchini mwao.
 “Tunaishauri Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) izitumie nafasi ambazo watanzania wanawakilisha nchi ili kutangaza vivutio vyake vya katalii”.

No comments:

Post a Comment