Sunday, October 21, 2012

YANGA YAITANDIKA RUVU SHOOTING MAGOLI 3-2 UWANJA WA TAIFA

Mchezaji wa timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam akimiliki mpira mbele ya beki wa timu ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii  jijini Dar es salaam, mpira umekwisha  timu ya Yanga imeifunga Ruvu Shooting  magoli 3-2, Goli la tatu la timu ya Yanga limepatikana katika kipindi cha pili cha mchezo huo baada ya kutoka uwanjani kwa mapumziko zikitoshana nguvu  kwa kufungana magoli mawili kwa mawili katika kipindi cha kwanza Mchezaji wa Yanga Jerrison Tegete akishangilia mara baada ya kufunga goli la pili katika mchezo huo na kufanya kipindi cha kwanza kumalizika timu zikitoshana nguvu kwa magoli, mpaka kipindi cha pili ambapo Yanga iliongeza goli la tatu na kufanya matokeo hayo kuwa 3-2
Mashabiki wa timu ya Yanga wakizikilizaia maumivu wakati timu yao ilipokuwa iko nyuma kwa magoli 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kukomboa magoli hayo  na kuongeza goli la tatu katika kipindi cha pili.Picha Kwa Hisani ya Full Shangwe Blog

No comments:

Post a Comment