Saturday, October 20, 2012

KATIBA MPYA IWALINDE WANAWAKE


 Na Lucas Raphael,Sikonge

Wanawake wa kata ya kitunda wilayani sikonge mkoani Tabora wamesema katiba mpya itakayo undwa ilinde kundi la wanawake wato nchini kutokana na kundi hilo kunyanyaswa na jamii inayo wazunguka.

Wakitoa maoni ya mabadiliko ya katiba mpya tume hiyo ilipo temb elea kata hiyo walisema kuwa kundi la wanawake likumb ana na changa moto mbalimbali za kijamii ikiwa na kunyanyaswa kijinsia na kundi la wanaume kwa ngazi mbalimbali.

Issa siraji Mohamedi (51) mkazi wa kata hiyo ali sema wanawake wengi husani vijijini wananyanyaswa na wanaume wao kutokana na kutofaham sheria zinazo walinda.

Alisema kuwa wanawake hupigwa,kubakwa ikiwa na kufanya kazi ngumu kila wakati hali ambayo wanawake hao hushindwa kujua haki zao wazipate wapi kutokana na kutofahamu sheria zao.

Issa akitoa maoni yake alisema kuwa katiba mpya itakayo undwa iwalinde wanawake ikiwa na kuwapatia elimu juu ya haki yao ili kutoa fursa ya kuwapatia haki za msingi ambazo wanapaswa kuzipata.

Alisema kuwa sheria kali ziwekwe za kuwa Linda wanawake kwa lika zote ikiwa na kuwabana wanaume wanao wanyanyasa wake hao.
Kundi hilo la wanawake katika mikutano mbalimbali ya kutoa maoni ya katiba mpya wanawake wamekuwa hawajitokezi kwa wangi ilikuja kutoa maoni yao juu ya katiba itakayo undwa.

Aginnes kapamila (56) mkazi wa kata hiyo kitoa maoni yake alisema kuwa katiba mpya iwalinde wanawake hasa kwa kuwaangalia kuwa wengi wao hawajitokezi kutoa maoni na mwanya huo usitumike kuwakandamiza.

Akibainisha changamoto zinazo wakabili wanawake kuwa ni pamoja na kufanya kazi ngumu,kubakwa,kunyimwa mirasi pamoja na kupigwa na waume zao ,Katiba hiyo izingatie mambo muhimu yanayo wagusa wanawake.

Mwisho.





No comments:

Post a Comment