Saturday, October 20, 2012

MAWASILIANO MAZURI KWA AJILI YA JAMII KUPATA HABARI


 Na Lucas Raphael,Tabora

Wananchi wa kata ya kipili wilayani sikonge mkoani Tabora wamesema katiba mpya izingatie mawasiliano ya miundombinu,simu pamoja na kupata mawasiliano ya vyombo vya habari kulingana na maeneo husika.

Wakitoa maoni ya katiba mpya pindi tume hiyo ilipo tembelea kata hiyo walisema kuwa mawasiliano ya simu yapewe kipaumbele kwa jamii ili kupata fursa ya kupata mawasiliano ya kupashana habari.

Wananchi hao wakizungumza kwanyakati tofauti walisema kuwa katiba izingatie mawasiliano ya jamii ili kila mwananchi wa Tanzania aweze kupata fursa ya kupashana habari na kupata habari kutoka eneo moja hadi eneo jingine.

Wananchi hao wa kata hiyo hawana mawasiliano ya simu,miundombinu mibovu wakati wa kipindi cha mvua pamoja na mawasiliano ya vyombo vya Habari haliambayo ilichangia wananchi hao kuomba katiba izingatie huduma hiyo hususani vijijini.

Emmanueli Ndege alisema kuwa katiba izingatie huduma hiyo muhimu kwa jamii ili wananchi wanufaike na fursa hii ya utandawazi tofauti na hali ilivyo sasa baadhi ya wananchi hawana mawasiliano.

“mawasiliano ni kitu muhimu sana kwa wananchi kwani eneo hili tunaweza tukapata majanga,ama matukio inakuwa ngumu kutoa taarifa lakini kama mitandao inakuwepo taarifa zina tolewa kwani kwa sasa simu zetu zinaozea mifukoni.’’alisema mkazi huyo.

Osca John akichangia maoni yake aliongeza kuwa endapo makuampuni yamawasiliano yanaingia mikataba na serikali yawekewe sheria ya kuhakikisha eneo husika wanapata mawasiliano kulingana na mikataba hiyo ilivyofungwa na sikwakuchagua eneo mmoja 

Tume hiyo ya katiba kundi la tisa la mkoa wa Tabora lilisafiri umbali wa kilometa 380 kuwafuata watanzania wa kata hiyo kutoa maoni yao juu ya katiba mpya ambapo tume hiyo ililazimika kufanya mkutano mmoja kulingana na changamoto za umbali pamoja na miundombinu.

Hata hivyo wananchi wa kata ya kipili na kitunda walisema kuwa viongozi wa kiserikali huwa hawafiki maeneo hayo kwanyakati mbalimbali mpaka matukio ya kitaifa yafike hali ambayo hujihisi kama wametengwa na serikali yao.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment