Tuesday, October 23, 2012

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR ATAKA WAZAZI KUWEKEZA KATIKA ELIMU

Balozi Seif Ally Iddy akizungumza na waandishi wa habari kwenye mahafari ya 10 kwenye shule ya sekondari ya Modern alipokuwa mgeni rasmi mwishoni mwa wiki.kushoto ni mkuu wa shule hiyo Philip Wasike. PICHA NA MAHMOUD AHMED
 ………………………………………….
Na.Ashura Mohamed-Arusha
 Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya  Zanzibar Balozi Seif  Iddi amewataka wazazi nchini kuwekeza katika sekta ya elimu ili watoto waweze kupata elimu bora zaidi kwa kuwa karne ya sasa ni tofauti na karne ya zamani.

 Aliyasema hayo katika mahafali ya kumi ya kidato cha nne,sita,darasa la saba,kidato cha tatu c katika shule ya Arusha Mordem iliyopo eneo la Kisongo nje kidogo mwa Jiji la Arusha.
 Balozi Seif alisema kuwa hii ni karne ya 21 ya sayansi na teknolojia ambapo elimu ni kitu cha thamani na kikubwa sana hivyo pindi mzazi anapokuwa amewekeza katika elimu kwa mtoto wake basi ni wazi kuwa mzazi anakuwa ameisaidia serikali kuandaa taifa ambalo si tegemezi.
 Pia Balozi Seif alikemea tabia ya viongozi kuingiza swala la siasa katika mambo muhimu kama elimu kwa kuwa inaondoa ufanisi katika sekta hiyo hivyo amewataka viongozi kutenganisha siasa na elimu kwa siasa kubaki siasa na elimu iwe ni elimu.

 Alisema kama siasa itaingizwa katika sekta ya elimu basi matokeo yake ni kuvurunda katika sekta hiyo hivyo ni lazima jitihada za makusudi zifanyike  ili kuzuia siasa katika sekta hiyo na iendelee kufanya vizuri ili Tanzania ipate viongozi bora wa baadae wenye elimu ya kutosha itakayoisaidia nchi kupata maendelao.

 “Mimi nataka niwaambie kuwa hakuna haja ya kuingiza maswala ya siasa katika sekta ya elimu ila siasa ibaki kama siasa alafu elimu pia ibaki kama elimu tukienda kwa mfumo huo tutapata mambo mengi mazuri ila tukiingiza siasa  sekta hii itavurugika na tusitegee chochote kipya”alisema balozi Seif

 Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo Philip Wasike alisema kuwa kuna uvumi ulionea kuwa shule ya arusha morden imefilisika na kuuzwa kwa taasisi moja ambapo amefafanua kuwa uvumi sio ukweli bali kilichofanyika ni kuwa kutokana na eneo la shule hiyo lilivyokaa imeonekana kuwa ni dogo hivyo uongozi wa shule hiyo umeamua kujenga compus nyingine katika eneo la njiro ambapo itagharimu jumla ya shilingi bil.6.

 Bw.Wasike alisema kuwa shule ya  Arusha Morden kwa sasa inafanya vizuri katika matokeo mbalimbali haswa katika mtaala wa Cambrige ambapo wanafunzi wamekuwa wakifaulu kwa kiwango kikubwa zaidi hivyo lengo la compus hiyo kuhamishiwa Njiro ni kuwa shule ya kipekee zaidi kwa kuwa shule hiyo kwasasa ina mitaala miwili ya baraza la mitihani Tanzania(NECTA) na Baraza la mitihani la uingereza(CAMBRIGE).

 Aliongeza  kuwa  bila kuwa na eneo la kutosha wanafunzi hawataweza kujisomea kwa nafasi ya kutosha kila mmoja kutokana na mtaala wake bila kuathiri wengine hivyo compus hiyo ya njiro inategemewa kumalizika na pindi ifikapo April 2013 compus ya kisongo itahamia njiro.

 Pia alitumia fursa hiyo kutoa changamoto kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi kujaribu kuangalia namna ya kuboresha mfumo wa elimu wa Tanzania ili uendane na karne ya sayansi na teknolojia kwa kuwa mfumo huo iliopo mpaka sasa umetumika kwa muda mrefu sana.

 Amesema kuwa mfumo uliopo wa elimu unaonekana kama ni wakukariri  hivyo ni lazima pafanye mabadiliko ili ueendane na wakati uliopo kwa kubadili aina ya ufundishaji  kwa sasa  ambao utamfanya mtoto afikiri zaidi ili uweze kumsaidia pia hata kutumia akili njyingi zaidi kufikiria maisha na kujitegemea bila kutegemewa kuajiriwa.
 Jumla ya wanafunzi 130 wamehitimu elimu ya msingi na sekondari  ambapo shule hiyo ina  wanafunzi  kutoka nchi kumi na mbili tofauti ndani na nje la bara la afrika

No comments:

Post a Comment